Nyaraka za URFIG – Uchangamuzi
kuhusu :
OMC
- Shirika la Biashara Ulimwenguni - WTO
Shirika la Biashara Ulimwenguni :
MILKI
YA MASHARIKI YAJIDHIHIRISHA
Kamwe ulimwengu waukukuwa totauti kama
ulivyo leo, mwanzoni mwa karne hili la 21. Kamwe shimo baina ya nchi tajiri na
nchi maskini halikukuwa pana kama lilivyo leo. Kamwe upana baina ya Kaskazini na
Kusini haukukuwa mkubwa kama ulivyo leo. Kamwe upinzani baina ya serikali za
kaskazini na za kusini haukukuwa wazi siku kwa siku, katika mwezi huu wa mwisho
mbele ya mkutano wa 4 wa mawaziri wa Shirika la Biashara Ulimwenguni
unaotarajika mjini Doha, huko Katar.
Bila shaka, kwanza nchi tajiri zitapaswa
kujibu juu ya hali hii ya hatari kwa binadamu. Kwa hiari nchi hizi zilipotosha
nafasi nzuri iliyosababishwa na mwisho wa vita baridi pamoja na kugawanya
ulimwengu katika makundi mawili ya kisera. Badala ya kuanzisha sera mpya ya
kimataifa inayoheshimu sheria na kusaidiana baina ya watu, sera ya ushindi ya
Marekani na Umoja wa Ulaya ilitawala. Katika filosofia hii twataja maafikiano ya
Marrakech yaliyotiliwa sahihi mnamo mwaka wa 1994 baada ya duru ya Uruguay.
Maafikiano haya hayana uhaki. Nchi maskini zalazimishwa kufanya mengi wakati
nchi tajiri hazipazwi kufanya lolote lile. Maafikiano haya yanatumika bila haki
katika Shirika la Biashara Ulimwenguni ambalo ni mtumwa wa nchi tajiri na
makampuni yake ya kimataifa.
Tangu mkutano wa Seattle, nchi maskini, wiki
baada ya wiki kuko mjini Geneva, zilipinga duru mpya ya mapatano ampayo
ingelilipa nguvu zaidi Shirika la Biashara Ulimwenguni. Nchi masikini ambazo zi
nyingi miongoni mwa nchi 142 ambazo ni wanachama wa Shirika hili zilihimiza
kutimilika kwa makubaliano ya Marakech : utathmini wa mapatano kufuatana na
mazingira mapya ya kijamii, ya kiuchumi na kitamaduni pamoja na kuandika upya
maafikiano haya kufuatana na masharti mapya. Zikiongozwa na Muungano wa Ulaya
pamoja na Marekani, nchi tajiri zilikata kata kata mapendekezo haya ya nchi
maskini.
Tarehe 19 Septemba, mjini Geneva, upinzani
huu umeonekana wazi. Marekani
imeuonesha kinaganaga. Kwa upande wake, katika waraka nafiki, Muungano wa Ulaya
umepinga marekebisho yoyote yale juu ya maafikiano yahusuyo haki za kitaaluma.
Marekebisho haya yalikuwa yanatakika katika nchi maskini kwa ajili ya kupata
madawa muhimu zaidi.. Nchi maskini zina lengo la kulinda faida nono ya makampuni
ya madawa.
Nchi tajiri zaficha kushindwa kwa sera zake
katika kundi la wengi duniani. Hali kadhalika, zinaendelea kifidhuli kutoa
hotuba za kupiga vita umaskini. Muungano wa Ulaya umeanzisha kampeni kubwa ya
kutetea duru mpya ya mapatano. Mapatano haya yangelihusu nyanja pana zaidi na
zingelieneza uhuru wa biashara usio na mipaka. Sera hili zingeliotesha mizizi
wale mwenye nguvu na kunyonga mwenye kukosa nguvu Uongozi wake wa Biashara ya
dunia si halili : unaweka dunia yote mikononi mwa makampuni ya kaskazini.
Bali nchi hizi hazikuwa tayari kwa upinzani
zinaokutana nao sasa : katika mkutano uliokuwa umeandaliwa mjini Geneva,
mwishoni mwa mwezi wa Juni na mwishoni mwa mwezi wa Julai, ilidhihilika kwamba
hakuna ukubaliano wowote ule kati ya nchi tajiri na nchi maskini juu ya nia ya
duru mpya. Mwishoni mwa mwezi wa Julai, kuhusu nyanja 20 ambazo Muungano wa
Ulaya unataka kuingiza katika duru mpya, hakukuwa na makubaliano licha ya nguvu
za aina zote zilizotumiwa na Kamati ya Ulaya pamoja na serikali fulani ambazo
zaficha kutokubaliana huku na kutoonyesha kwa wananchi wake sera zake za ukoloni
mambo leo. Mwishoni mwa mwezi Julai, mataifa 49 ambayo ni maskini zaidi, katika
mkutano wake huko Tanzania, zimeonyesha upinzani wake juu ya duru mpya. Tarehe
24 Septemba, mjini Abuja (Nigeria), licha ya mbinu zilizotumiwa hasa hasa na
Kamati ya Ulaya kwa ajili ya kushawishi nchi maskini, mawaziri wa kiafrika ,
wote kwa pamoja, wamepinga upya duru hii.
Afrika yasema kwamba nchi za kiafrika
hazitaki mapatano mapya ya kimataifa juu ya nyanja mpya ; hazina uwezo wa
kutimiza masharti yatakayotokana na mapatano haya ; hazioni faida
zitakayoitoa kwenye kuhurisha biashara ya nyanya mpya ; zina mashaka juu ya
masharti zaidi, tena zinaogopa hatari ambayo ingesababishwa na kuongezeka kwa
uwezo wa Shirika la Biashara Ulimwenguni ; hakuna makubaliano baina ya nchi
wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni juu ya kuanzisha mapatano ya namna
hii na makundi tofauti ya kikazi ndani ya Shirika la Biashara Ulimwenguni hayana
budi kuendeleza zaidi uchunguzi katika uwanya huu.
Barani Asia, Inda imeeleza upya upinzani wake
juu ya duru mpya. Katika mkutano wake wa tarehe 28 Septemba mjini Bangkok,
mataifa 33 ya Asia na Pacifika yamelaumu ukosefu wa uangavu katika nyaraka
zilizoandaliwa na Shirika la Biashara Ulimwenguni kwa ajili ya mkutano wa
mawaziri ujao. Mataifa haya yalisema kwamba yangelipenda zaidi makubaliano mapya
juu ya mapatano ya Marakech kuliko duru mpya.
Muungano wa Ulaya hauna la kusema juu ya
upinzani huu. Marekani
na nchi tajiri vile vile. Wanahabari wanawaunga mkono katika kuficha msimamo huu
wa nchi maskini. Wananchi hudanganywa kwamba sera zake zakubalika katika nchi za
kusini na kwamba upinzani unaosikika ni wa Wanaulaya na Waamerika wasio na
dhamana ambao wanashughlikia maNGO’s.
Ni
kweli kwamba tangu siku chache twasikia vyama fulani vyenye siasa za kijamii na
kidemokrasia vikisema eti vinataka « utu zaidi katika utandalizi ».Vyama
hivi vyaogofywa na mafanikio ya maandamano yanaopinga utandalizi. Walakini vyama
hivi vinaendelea kuunga mkono Kamati ya Ulaya ambayo inafanya kazi kinyume na
sera zinazoanza sasa kutetewa na vyama hivi. Utu huu ni kama ule wa watetezi wa
ukoloni ule wa wenye kuviunga mkono vita vya kikoloni. Utu hauwezi kuwa ile
imani ya kifidhuli iliojiita « kazi ya Ulaya ya kustaarabisha »
Tareha
26 Septemba, nchi tajiri zilipanda hatua zaidi. Ziliandika kwa kutumia mikono ya
Shirika la Biashara Ulimwenguni nyaraka mbili zenye kudhaminika kwa nchi hizi
kupitishwa katika mkutano ujao wa mawaziri. Waraka wa kwanza ni taarifa la
kiwaziri ambalo lingelifungua rasmi duru mpya. Taarifa hili halizingatii
mapendekezo ya nchi za kusini. Katika taarifa hili kumeandikwa mapendekezo yote
ya nchi tajiri. Waraka wa pili unazingatia mbinu dhaifu dhaifu ambazo
zingelitumia kwa kuchunguza njia za kutimiza maafikiano yaliopo.
Katika
nchi maskini nyaraka hizi zilionekana kama matusi. Tarehe 2 oktoba, kwa niaba ya
nchi 49 maskini zaidi, marozi wa Tanzania kwenye Shirika la Biashra Ulimwenguni
alikumbusha kwamba nchi maskini haziwi tayari kwa duru mpya. Barozi alisema
kwamba nchi hizi hazina uwezo wa kushiriki katika mapatano haya na kwamba zakosa
uwezo wa kutimiza masharti ambayo yangelisababishwa na mapatano haya. Barozi wa
Malaysia alitaka nchi tajiri ziache kushawishi kwa nguvu nchi maskini.
Bwana
Pascal Lamy ambaye ni Kamishna wa Ulaya, bila shaka akihimizwa na hali ya
ulimwengu leo, bila kutabasamu, tarehe 1 oktoba, alitangaza : « Duru
mpya ingesaidia katika kupiga vita ugaidi ».
Unafiki
wa nchi za Ulaya wakosa mipaka. Hotuba nzuri za kupiga vita umaskini zatolea na
serikali zetu, wakati kwa upande mwingine serikali zizi hizi, kwenye pahali pa
kutolewa uamuzi, huwa na misimamo ambayo huongeza zaidi umaskini na hali ya
kutegemea nchi za kaskazini kwa nchi za kusini.
Bila
kukawia, hatuna budi kukumbusha wajibu wake kila mbunge na kila waziri wetu.
Kwani, hatimaye, sera za Muungano wa Ulaya na za Shirika la Biashara Ulimwenguni
huamuliwa katika kila nchi mwanachama.
Dr
Raoul Marc JENNAR
Mtafiti
kwenye Oxfam Solidarité (Brussels) na kwenye URFIG (Paris)
9 oktoba 2001