URFIG – Habari za Afrika
Tarehe 25 mei, Jubilii 2000/Shirika
linaloshughlikia madeni na maendeleo Afrika (CAD-Mali) pamoja na shirika la
wanafunzi wa kiafrika huko nchini Mali (CONEAM), yamesherehekea siku kuu ya
Afrika
Alhamisi 24 mei 2001, kati ya saa tatu asubuhi na saa moja jioni, katika
jumba Mémorial Modibo Keita, CAD-Mali na CONEAM yameandaa semina ya kuimarisha
uwezo wa vijana barani Afrika.
Semina hii ilikuwa na lengo la kufunza na kubadilishana mawazo. Wakufunzi
123 kutoka vyuo na vyuo vikuu tofauti vya Mali na wanayoyawakilisha mataifa 17
ya bara la Afrika, yaani Niger, Kameruni, Burkina Faso, Ivory Coast, Benin,
Visiwa vya Komoro, Moritania, Kongo Brazzaville, Kongo Kinshasa, Togo, Djibuti,
Afrika ya Kati, Gabon, Chadi, Guinea Konakri, Madagaska na Mali, waliyahudhuria
mafunzo haya.
SHABAHA KUU LA SEMINA
Kuhimiza na kuhamasisha wanafunzi wa kiafrika wanaoishi nchini Mali, ili
waibuke makada wa kiafrika angalifu na wenye busara, walio tayari kutetea haki
za kiuchumi jamiini.
SHABAHA DHAHIRI
Kufunza viongozi wa makundi ya wanafunzi, watakaoendelea kazi ya kuhimiza
na kuhamasisha wenzao ndani ya makundi watokamo.
AJENDA YA SIKU YA
KUBADILISHANA MAWAZO
Mada : Maendeleo ya Afrika –
Madeni na Ujana
I. Asili ya
kihistoria na ya kisasa ya mgogoro wa madeni
A . Ya
kihistoria :
Urithi
wa utumwa na ukoloni, mbinu za unyonyaji na udhibiti wa mataifa ya Afrika.
B. Asili
za nje za kisasa :
-
Uharibifu wa hali ya mabadilishano ya kiuchumi
-
Migogoro ya mafuta (petroli)
-
Kushuka kwa kiwango cha riba na cha kubadilisha fedha za
kigeni
C. Asili
za ndani za kisasa :
-
Uongozi wa sekta ya umma, udhaifu wa kujiweza na ulaji
rushwa
-
Ratiba mbovu za maendeleo ambazo hazizai matunda
II. Utatuaji wa
migogoro
A.
Ratiba
za marekebisho ya miundo (structural adjustement programs) :
-
Misingi ya kinadharia (mawazo ya uwanja huu)
-
Shabaha za ratiba za marekebisho ya miundo
-
Utathmini wa uhakiki
B.
Siasa ya kupunguza madeni
(Kufeli
kwa siasa za marekebisho na za kuahirisha madeni)
-
Hatua za pande mbili
-
Hatua za pande mbili (hatua HIPC ya asili na ile
iliyesahihishwa, CSLP)
-
Mtindo wa soko (ubadilishaji, ufitaji wa deni nk.)
III. Maendeleo ya
Afrika, madeni na ulimwengushaji wa mambo ya dunia (Mondialisation)
A.
Mmomonyoko wa wajibu wa serikali na kuharibika kwa jamii (ukosefu wa kazi,
umaskini, hali isiyo ya usalama nk.)
B.
Maendeleo yanayohimizwa na hali ya soko
C.
Shughli pevu za kuanzisha upya ukoloni (ubinafsishaji
wa mali ya umma, ulegezaji wa masharti, kutotiisha sheria nk.) na za
kurudisha hali ya utumwa
IV. Ujana
-
Kuna mtazamo sahihi gani kwa ajili ya maendeleo ya vijana wa
kiafrika
-
Ili maswali yote haya yaliyotajwa yawe na jibu, wanafunzi
walisema nini ?
V. Hitimisho
Kwa ajili ya mtindo mwingine wa maendeleo.
Sherehe za kufungua na kufunga semina ziliongozwa na Bibi BARRY Aminata
Toure, mwenyekiti, Bwana DAO Dounantie, katibu mkuu na Bwana Ibrahim Hamani
Souley, katibu mtendaji wa CONEAM.
Hotuba ya mwanzo ilisomwa na Bwana Sékou DIARRA, mkufunzi. Hotuba hii
ilikuwa inahusu hasa hasa ajenda ya semina. Baada ya hotuba hii wanafunzi
waliunda makundi manne. Kila kunda lilipewa mada ya kujadili.
Vile vile, kila kundi (likiungwa mkono na mwanachama wa CAD-Mali)
lilikuwa na wajibu wa kubadilishana mawazo na kufasiri mada ndogo moja kwa ajili
ya kuielewa vizuri na kuibuni mitazamo sahihi.
Baada ya kazi ya makundi, washiriki wote walikutania upya ndani ya chumba
cha mkutano. Pale, kila kundi liliwasilisha uchangamuzi na mitazamo yake.
N.B :
Katika siku za usoni tutawatumia ripoti ya kinagaubaga ya semina ya kufunza na
kubadilishana mawazo, ili mtukosowe na mtupe mapendekezo yenu.
CAD-Mali linataraji kuandaa mkutano wa mamna hii tarehe 09/06/2001.
Katika shughli hii CAD-Mali litashirikiana na makundi na mashirika ya wanawake (CAFO).
Kwa
niaba ya uongozi
Katibu
Mkuu
Ofisi
ya taifa ya CAD – Mali inayoshughlikia PPTE na umaskini nchini Mali
Bibi
Barry Aminata Touré
Internet na E-mail ya bure Alta Vista http://www.altavista.fr
E-mail
: samba@altavista.fr
Jubilé
2000/Coalition des Alternatives Africaines Dette et Développement (C.A.D-Mali)
en collaboration avec la Conférence des Etudiants africains au Mali (CONEAM)
ont commémoré le 25 mai, journée historique de l'Afrique