URFIG – Habari za Afrika
Bunge la Kenya lapitisha muswada wa sheria
kuhusu madawa ya UKIMWI
(12 Juni 2001)
NAIRIBI (Reuters) –
Jumanne, Bunde la Kenya limepitisha muswada wa sheria wenye utata. Muswada huu
ulipingwa na makampuni makuu ya dawa yanayoruhusu nchi hii ya Afrika ya
Mashariki kuingiza na kutengeneza madawa rahisi.
Wabunde, wote kwa pamoja,
wamepiga kura na kukubali muswada wa sheria unaohusika (Industrial Propeties
Bill 2001). Hivi, walilegeza mamlaka ya makampuni makubwa ya madawa, yenye hati
za haki zinazothaminiwa sana juu ya madawa tofauti, kukiwamo yale yanayopunguza
ukali wa virusi vya UKIMWI.
Wahamasishaji wanaopiga vita
UKIMWI wanasema kwamba kufuatana na muswada huu, zaidi ya miliyoni 2.2 za
Wakenya wenye virusi vya UKIMWI watapata madawa ambayo, katika Nchi za
Magharibi, yalipunguza vifo vinavyosababishwa na UKIMWI kwenye kiwango cya
asilimia 75.
Kenya
ni nchi ya pili ya kiafrika inayopitisha muswada wa namna hii. Mnamo mwezi wa
Aprili, nchini Afrika ya Kusini, makampuni ya madawa yalipoteza nguvu wakati
yaliamua kuacha ushtaki mahakamani dhidi ya muswada wa sheria unaofanana na huu.
"Hii ni siku kuu, siku kuu sana",
aliambia Reuters Bwana Sam Ongeri, Waziri wa Huduma za Afya kwa Wananchi. "Wakenya wanaweza kutabasamu, sasa wana uwezo wa kujinunulia madawa
rahisi, bali bora".
Walakini
itachukua muda kidogo kabla ya madawa rahisi haya kuingizwa nchini Kenya kwa
jumla. Inabidi muswada urudi bungeni na kusoma upya. Pale marekebisho madogo
madogo huenda yatajadiliwa. Bali kiini chenyewe cha sheria hakiwezi
kubadilishwa. Baadaye, ridhaa ya rais itahitajika.
Kufuatana
na muswada wa sheria, Kenya itayapa notisi ya miezi sita makampuni ya madawa ya
kimataifa yenye kumiliki hati za haki, ikiwa inataka kutoa kwa makampuni mengine
vibali vya kuingiza ama kutengeneza madawa ya ainasafu.
Makampuni
yanaogopa kwamba nchi nyingine za Afrika zinaweza kufuata nyayo za muswada huu
na kuondoa faida ambayo, kwa niaba ya makampuni haya, ni muhimu kwa utafiti wa
madawa mapya. Katika bara hili watu miliyoni 25.3 wana virusi vya UKIMWI.
Lakini, kwa upande mwingine, Bwana Ongeri anadhani makampuni ya madawa hayangelikuwa "na busara" yangelishtaki kwenye mahakama ya Kenya muswada huu. "Haingeenea kwenye hali ya taifa", alisema Waziri.