HABARI ZA DOHA
INGAWA KUNA BREKI,
(Dr Raoul Marc JENNAR
Kama ilivyokuwa katika mkutano wa
Marrakech, katika mkutano wa Doha, nchi tajiri hazikulegeza sera yake ya
kulazimisha dunia nzima kufuata mfumo mkali wa huria ya kibiashara. Walakini,
tangu 1994, mwishoni mwa duru ya Uruguay, wakati yalipopitishwa maafikiano mengi
ya Shirika la Biashara Ulimwenguni, sera hii haikuridhisha wale wote
wanaopendekeza hasa, ili umaskini upunguzike, kugawana ifaavyo mali inayozaliwa,
usawa wa haki na kutovunja haki za kila jamii juu ya maslahi binafsi.
Kila mwaka, vionyesho vyote vya
kiuchumi vinathibitisha kwamba huria ya kibiashara, inayopendekezwa, inanufaisha
nchi tajiri peke yake. Kutowahi kuamua kitu katika mkutano wa mawaziri wa
Seattle kulihimiza nchi za Kusini kupinga nia ya ubeberu wa nchi za Kaskazini.
Kutokana na maendeleo thabiti, katika nyanja za ustadi, ya nchi zinazoengelea,
pamoja na mshikamano wa maoni ya nchi hizi, mkutano wa Doha, ingawa ulianzisha
upya duru ya biashara ya bidhaa na huduma, ulipunguza tamaa ya nchi tajiri.
Bali, kazi yenyewe ya mkutano wa Marakech haikukataliwa. Hali kadhalika, itabidi
kuwe na juhudi mpya zaidi, ili upinzani wa nchi zinazoendeleo uwe na msimamo
imara katika mkutano wa mawaziri utakaofanyika mnamo miaka miwili. Baadhi ya
dharura za nchi tajiri zinatarajika kujadiliwa katika mkutano huu.
Mkutano wa Doha ulikuwa pia somo kwa
Wanaulaya wanaopigania kuwepo kwa dunia halali, inayoheshimu haki.. Dunia yote
ilitambua unafiki na kuwa na ndimi mbili kwa serikali za Ulaya na Kamisheni ya
Brussels. Hotuba za kiutu na ukarimu, zenye lengo la kutuliza wazalendo wema wa
kiulaya na kutumia vibaya uaminifu wa baadhi ya serikali za kusini, bado
hazijajithibitisha katika mapatano. Ukweli ni kwamba Ulaya unakuwa kwenye upande
wa Marekani, siyo kwenye upande wa nchi zinazoendelea : sera ya kulinda
viwanda vya nchini inapitishwa ikiwa tu inaridhisha nchi tajiri.
Hivyo, wajidhihirisha wajibu wa
serikali 15 za kiulaya pamoja na vyama vya kisiasa vinavyoziunga mkono. Serikali
zote za kiulaya, ikiwa ni ile ya Jospin au ya Berlusconi, zi pamoja katika
kuunga mkono uwezo na kazi ya Pascal Lamy. Kwa bahati mbaya, kushiriki katika
serikali nyingi kwa Wakomunisti au kwa wateteaji wa mazingira, hakukubadili
kitu.
Kutokana na kuwa katika mkutano wa
Doha wananchi hawakuweza kubadili uwezo uliopewa Kamisheni ya Ulaya na mabunge
15 ya kitaifa pamoja na serikali 15 vile vile tangu mkutano wa Seattle, inafaa
zibuniwe mbinu za kutumia katika miezi ijayo. Hali serikali za kiulaya na vyama
vinavyoziunga mkono zilivyoonyesha kuridhika kwake huko Doha kwatuonyesha njia
ya kufuata.
NAMNA YA KUAMUA : BADO UKO
UKIRITIMBA WA WATU WACHACHE
Nchi zinazoendelea zilionyesha
jitihada kubwa katika kuandaa mkutano wa Doha. Jitihada hii ilionekana pia
katika kufafanua mambo na kufasili maoni na mapendekezo. Nchi hizi zilijadili
kidemokrasia, kinyume na Wamarekani na Wanaulaya wanaojidai kuwa waalimu wa
Demokrasia. Wamarekani na Wanaulaya walitumia nguvu zote ziwezekanazo ili
mkutano wa Doha uanze watakavyo, bila kujali kufuata kanuni za Shirika la
Biashara Ulimwenguni.
Misimamo
iliyotangazwa na nchi zinazoendelea katika mikutano mingi ya kimataifa [mikutano
ya nchi za kiafrika, kundi la Afrika Karibean na Pasifika, nchi zinazoendelea,
kundi la nchi 77] au katika mikutano rasmi au la ya Shirika la Biashara
Ulimweguni, haikuzingatiliwa au ilikanwa. Vyombo vya habari vya magharibi
viliunga mkono serikali zake vikikataa kusema kitu juu ya maoni yaliyokwenda
kinyume na maoni nchi tajiri zilizotaka kupitisha kwa nguvu.
Miswada
tofauti ya taarifa ya mawaziri iliyoandaliwa na Halimashauri kuu ya Shirika la
Biashara Ulimwenguni ilitegemea kikashfa upande mmoja. Bila kujali uvunjaji wa
kanuni za shirika hili, miswada hii haikugusia misimamo ya nchi zinazoendelea.
Tangu walipofika Doha, wajumbe rasmi walilazimishwa kujadili juu ya mswada wa
taarifa ulioamriwa na nchi tajiri. Inajulikana wazi kwamba unapojadili juu ya
maoni ya mpinzani wako, unajiweka katika hali ya udhaifu.
Huko Doha, maandalizi ya kazi
hayakujali kanuni za kimsingi za udemokrasia katika mijadala. Kinyume, sikio
lilitegwa mwenye nguvu. Nguvu hizi zilitumika vile vile katika mikutano ya nchi
kwa nchi baina ya nchi tajiri na nchi zinazoendelea. Ahadi,
kama vile hamanisha, ilitumiwa. Watu walioteuliwa, ili waendeshe
mashauriano kwa niaba ya urais, walichaguliwa katika wafuasi wa sera za nchi
tajiri. Hali kadhalika, nyanja zilizochaguliwa kujadiliwa ni zile zinazozingatia
mapendekezo ya nchi zizi hizi.
Nchi
zinazoendelea zilipigania kuingizwa kwa mjumbe wake katika wawakilishi hawa
waliojadili juu nyanja zinazopendekezwa na nchi hizi.. Ingawa mapatano
yalifanyika katika makundi saba, jambo ambalo lisingeliwezekana bila kuwepo kwa
ujumwe mkubwa kwa kila nchi, mashauriano haya, kama vile mikutano ya wakuu wa
ujumbe, ilizipa nchi maskini fursa ya kuifanya sauti yake isikike.
Hii
ni hatua nzuri iliyofanyika, kinyume na wakati wa mkutano wa Seattle, ambapo
wajumbe wa nchi maskini, -ingawa wajumbe hawa walikuwa wengi kuziidi wengine-,
walikuwa wanangonja vishorobani kukubaliana kwa wajumbe wa nchi tajiri waliokuwa
wanaendesha mapatano kati yao.
Katika
mkutano wa Doha, nchi tajiri hazingelijaribu kuweka kando nchi maskini na
kujadiliana kati yake bila kupotosha mkutano kama ilivyokuwa katika mkutano wa
Seattle.. Si rahisi kutenga nchi yenye biliadri ya wakaaji, kama ilivyo India.
Ndiyo maana mbinu zote za ustadi wa shughli zilitumiwa.
Ilipogunduliwa
kwamba nchi maskini zilikuwa na uwezo wa kulazimisha nchi tajiri kuacha baadhi
ya mapendekezo yake, « mashauriano yasiorasmi » yalianzishwa upya.
Mbinu hizi zilitumiwa vile vile katika mikutano ya Marrakech na Seattle, kama
zinavyotumiwa katika kazi ya kila siku ya Shirika la Biashara Ulimwenguni. Mbinu
hizi zajulikana kwa jina la utaani la « green room », kutokana na
rangi ya awali ya chumba cha ofisi ya mkurugenzi mkuu wa Shirika la Biashara
Ulimwenguni.
Chumba
« green room » cha Doha kilikuwa ni « chumba kibubwa cha
kirais n° 11.» Hapo ndipo kundi la wanamagharibi na marafiki zake
walipokutania katika mara tofauti na wajumbe wa nchi zenye msimamo mkali kuliko
nyingine. Katika usiku wa maamuzi wa tarehe 13 na 14 Novemba, mbinu hii
ilitumiwa pia kwa ajili ya kuweka India kando ya wajumbe wengine. Usiku huu ndio
ulioathiri mwelekeo wa mkutano wa Doha
Shughli
zilizofanyika tangu juma nne saa tatu usiku na juma tano saa 11 asubuhi
ziliendelea kwa kuvutia. Nchi 20 tu (juu ya 144 kutokana na kuwa Uchina na
Taiwan ziliteuliwa kuwa wanachama mnamo mkutano wenyewe) zilikubaliwa kuingia
katika chumba n° 11. Nchi nyingine zilizotaka kushiriki hazikukubaliwa
kuingiamo. Baadhi ya nchi zilizokubaliwa kuingia ziliruhusiwa kuwakilishwa na
waziri wake peke yake. Waziri hakukubaliwa kuwa pamoja na mtaalamu wa kumshauri.
Wenye kuendesha shughli hizi walichanganyisha nchi zilizoshiriki wakitumia
maandiko ya kujadiliwa. Ili mswada uwahi kupitishwa, washawishi walikuwa
wanaahidi :msaada wa kiufundi au walitisha kusimamisha msaada huu. Mawaziri
« wakaidi » hata waliogofywa na kuteswa. Katibu wa Shirika la
Biashara Ulimwenguni aliunga mkono namna hii ya kutenda, bila kujali wajibu wake
wa kufanya kazi kwa ajili ya wanachama wote.
Ni
baada ya usiku ule ulipomomonyoka umoja kati ya nchi za kiafrika, nchi za Afrika
Karibean na Pasifika na nchi maskini. Nchi za Afrika Karibean na Pasifika
zilikuwa zimekubaliwa kufuata watakavyo mfumo maalum wa kibiashara, kufuatana na
maafikiano ya Cotonou.
Walakini,
ingawa kulikuwepo vitendo hivi vya kimafia, vitendo ambavyo havishangazi
kujitokeza katika uwanja wa biashara, viitendo vilivyoungwa mkono na Serikali
zetu, katika masaa ya mwishoni mwa mkutano ulioongezewa muda wa siku moja, nchi
kumi zilikuwa bado na msimamo wake imara kabla ya kukutana kwa viongozi wa
wujumbe. Nchi hizi zililegeza msimamo wake zilipotishwa kujibu peke yake mkutano
ukifeli, kama ulivyofeli huko Seattle. India tu ndio ilioendelea kupigana vita
hadi mbali iwezekanavyo. Hatimaye, nchi hii ilikubaliwa ufafanuzi thabiti juu ya
mwanzo ulioahirishwa wa mapatano yahusuyo nyanja zilizoitwa nyanja za Singapore
(jambo hili litarudiwa). Ndiyo maana gazeti la kifaransa « Le Monde »
lilidharau nchi hii, eti « nchi hii ilijaribu kuwa kizuizi hadi mwishoni. »
Doha
ilionyesha wongo wa maandiko yaliyotangazwa hivi karibuni, tarehe 09.11.2001, na
gazeti Financial Times. Gazeti liliandika kwamba « mfumo wa kimataifa
wenye misingi ya kikanuni unawapa maskini na wenye kukosa nguvu haki
zinazofanana na zile zinazopewa matajiri na wenye nguvu ». Shirika la
Biashara Ulimwenguni lakosa demokrasia. Mfumo wa Shirika hili waheshimu mwenye
nguvu sio sheria. Sharti Shirika la Biashara Ulimwenguni lirekebishwe bila
kukawia. Kudharauliwa kwa nchi zinazoendelea kungelihimiza nchi hizi kuomba vya
kipaumbele marekebisho haya katika mkutano ujao wa mawaziri.
TAARIFA YA DOHA
YENYEWE : YOTE YAMO, ISIPOKUWA MAENDELEO
Ili « Taarifa ya
Doha» ieleweke vizuri, bora kukumbuka kwamba kuna aina mbili za mapatano katika
Shirika la Biashara Ulimwenguni. Kufuatana na Maafikiano ya Marrakech, kuna
nyanja ambazo hujadiliwa kadri kwa kudumu : kilimo, huduma na haki ya kazi
za kitaaluma. Hii ndio « ajenda ya daima. » Kuwepo au kusiwepo
mkutano wa kiwaziri, kuwepo duru mpya au la, mapatano katika nyanja hizi
yamepangwa na yanaendelea kufanyika. Uamuzi wa mkutano wa mawaziri ndio tu
unaokuwa na uwezo wa kusimamisha mapatano haya, kuyapunguzia uwezo au kuyapa
mwelekeo mpya. « Taarifa ya Doha » hufafanua mielekeo ya mapatano
juu ya nyanja hizi tatu.
Hivyo, dhaana
yenyewe ya « duru mpya » ina sasa lengo la mapatano juu ya nyanja
nyingine, totauti na nyanja hizi. Katika ratiba ya Doha kuna ajenda ya daima,
kuna vile vile duru mpya ya mapatano.
Katika majira ya
kuchipua jana, huko Uswidi, kulikuwepo mkutano wa wakuu wa Marekani na wa Ulaya.
Katika mkutano huu serikali za shirika hili la kiuchumi baina ya nchi jirani za
Atlantiki ziliwishi kuwepo kwa duru mpya kubwa ya mapatano. Mapatano ya namna
hii yangeliruhusu kunafisishwa kwa nyanja mpya ambazo kawaida zina uhusiano na
maisha ya kijamii. Tarehe 29 Oktoba, nchini Luxamburg, serikali 15 za kiulaya
ziliunga mkono kuwepo kwa duru kubwa. Wiki chache zilizopita, huko Singapore,
katika mkutano, usiokuwa rasmi wa nchi 20, kutokana na upinzani wa nchi
zinazoendelea, mpango huu ulipewa jina mpya la « ajenda ya maendeleo ».
Jina hili mpya halikubadili kitu juu ya mapendekezo makali ya kunafisisha
biashara.
Mpango wa Doha, iwe
ajenda ishirikishayo au duru mpya, si mkubwa wala wa kimaendeleo. Mpango huu
unazingatia tu makubaliano machache ya nchi tajiri, bila kufungulia milango
mapatano juu ya mapendekezo ya nchi zinazoendelea. Kama alivyoandika Chakravarti
Raghavan katika SUNS (n° 5011 ya tarehe 16 Novemba 2001), twaweza kuita duru
hili « duru la kila kitu isipokuwa maendeleo. »
Kanuni ya kwanza na
ya pili za Taarifa zathibitisha uzuri wa biashara yenye uhuru wote. Kwa niaba ya
wateteaji wa taarifa hii, biashara yenyewe ya namna hii ingeliboresha hali ya
uchumi na maendeleo. Wote walijivuna eti wanataka kupiga vita umaskini. Neno
hili liligeuka kama wimbo wa mashirika ya kimataifa (Benki ya Dunia, Sanduku la
Kimataifa la Fedha na Shirika la Biashara Ulimwenguni). Jambo la kushangaza ni
kwamba ni mashirika haya yaliyosababisha hali ya leo ya umaskini.
AJENDA YA DAIMA
Mapatano juu ya
nyanja tatu zinazohusu ajenda hii hudumu na kuendelea kwenye makao ya Shirika la
Biashara Ulimwenguni mjini Geneva. « Taarifa ya Doha » ilionyesha tu
mielekeo ambayo ingelifuatiliwa na mapatano haya. Kinyume na ombi la nchi
zinazoendelea, taarifa hii haikukosoa kamwe maafikiano yanayohusika.
Kilimo
Wengi mno kati ya
binadamu duniani wahusika na uwanja huu, yaani wakulima wadogo wadogo. Uwanja
huu wadhihirisha unafiki wa Muungano wa Ulaya na Marekani. Kila mwaka, Muungano
wa Ulaya na Marekani hutumia biliardi 380 za dola ya Marekani kama lipo au
msaada wa aina mbalimbali. Nchi zizi hizi, zikirejesha kwenye Maafikiano juu ya
Kilimo, huzuia nchi nyingine zote duniani kusaidia kilimo pamoja na uzalishaji
wa bidhaa za ulimaji (ikiwa nchi hizi zina uwezo wa kutekeleza jambo hili). Nchi
hizi huzuiliwa pia kulinda masoko yake ya ndani dhidi ya mchuano huu ambao si
halali.
Doha haikuwapa kitu
wakulima wadogo wadogo. Wakulima hawa hawakupewa kitu juu ya kilimo, juu la
kulinda rasilmali ya asili au ujuzi wa kienyeji (tazama majadiliano juu ya
Maafikiano kuhusu Haki za Kitaaluma -ADPIC). HAPANA KITU. Muungano wa Ulaya
ulijaribu hata kuufanya ufeli mkutano wa Doha kwa ajili ya kulinda viwanda vya
ulimaji barani Ulaya. Matunda ya uzalishaji wa hali ya juu wa bidhaa za kilimo
barani Ulaya yajulikana : dioxine, ng’ombe wenye wazimu, maradhi ya homa
ya mifugo, uchafuzi wa mazingira wa hali ya juu.
Nchi zinazoendelea
zilikuwa zinaomba kuandikwa katika maafikiano juu ya kilimo kwa sura maalum
inayohusu viwango vya ushuru wa forodha ya upendeleo pamoja na uamuzi halisi juu
ya ulimaji mdogo mdogo. Muungano wa Ulaya ulipinga sana ombi hili lijulikanalo
kama « Development Box ».
Katika mswada wa
taarifa kulikuwa kumeandikwa kwamba ingefaa « kuwepo kwa mapatano ya jumla
kwa ajili ya kupungua misaada kwa usafirishaji wa bidhaa nje, na kusimamisha
baadaye, hatua kwa hatua, misaada hii ». Kutokana na kuwa misaada ya Muungano
wa Ulaya i tofauti na ile ya Marekani, Muungano wa Ulaya ulipendekeza na
kukubaliwa kuandika usahihi kwamba kupungua misaada kungehusu « aina zote »
za misaada. Walakini, kwa upande mwingine, Muungano wa Ulaya ulikubaliwa
kutokuwa na maana kwa maneno « na kusimamisha baadaye, hatua kwa hatua,
misaada hii » kwa sababu, kabla ya maneno haya, kuliandikwa « bila kuenda
kinyume na matokeo ya mapatano yenyewe ».
Huduma
Taarifa ya Doha
inathibitisha mapatano yaliopo, mielekeo iliyoamuliwa na shabaha
linalofuatiliwa. Ingawa wananchi walifasiri woga wanao, hakukuwa na uamuzi
thabiti wa kulinda huduma kwa umma dhidi ya haja ya unafisishaji. Aya ya 7 ya
Taarifa ndiyo peke yake inayoeleza : « Kutokana na Maafikiano ya
jumla juu ya Biashara ya Huduma, tunathibitisha mara nyingine haki ya Wanachama
ya kujitungia sheria kuhusu utoaji wa huduma, na kujibunia sheria mpya katika
uwanja huu. »
Watu wengi huamini
kuwa aya hii itaziruhusu nchi kulinda dhaana ya huduma kwa umma, hasa hasa
katika nyanja za elimu na afya. Isisahaulike kwamba katika mapatano juu ya
mazingira ambayo yataanzishwa hivi karibuni (tazama chini) kuna huduma kwa
mazingira ambayo moja kwa moja yanawekwa hatarini na unafisishaji.
Haki
za Kitaaluma (ADPIC)
Maafikiano
juu ya Haki za Kitaaluma katika Biashara (ADPIC) – Fani iliyofasiriwa mno
katika Sheria ya kumiliki – huenda kinyume na haki za kimsingi : haki kwa
afya (A) na haki za kila jamii kwa kuwa na uhuru juu ya asilimali yake ya
kiasili (B), haki hii ikiwa tena inatiliwa mkazo katika maandiko ya sheria ya
kimataifa, maandiko ambayo yalipitishwa na kuidhinishwa rasmi na nchi zote.
Maafikiano haya juu ya haki za kitaaluma hugusia nyanja nyingine za kumiliki
kitaaluma (C).
A.
Kuhusu haki kwa afya na haki kwa madawa ya kimsingi, Taarifa pekee ilipitishwa.
Kupitishwa kwa taarifa hii kulitokana na juhudi ya Nchi Zinazoendelea. Nchi hizi
zilikuwa na msimamo mmoja imara katika vita hivi ambavyo kikweli vilikuwa vya
« kufa au kupona ».
Mnamo
mwezi wa Februari wa 2000, katika Bunge la Ulaya, Kamisheni wa Ulaya wa Biashara
ya kimataifa, kwa sauti ya kuamrisha, alihakikisha kwamba haki za kitaakluma
(hati) haziathiri bei ya madawa.
Taarifa
iliyopitishwa Doha yaonyesha kinyume. Yaliofanyika mpaka sasa yalichunguzwa.
Maandiko ya Doha juu ya « Maafikiano juu ya Haki za Kitaaluma na Afya »
ya hatua kubwa ya kisiasa, lakini yakosa nguvu za kisheria. Mara nyingi ukosefu
huu ulitiliwa mkazo na ujumbe wa Marekani.
Matatizo
yanayosababishwa na hati katika nyanja za afya ya umma na kukomesha magonjwa ya
mlipuko yalitambuliwa na kukubaliwa. Nchi ziliwishi kwamba Maafikiano juu ya
Haki za Kitaaluma yasizuie Wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni kutumia
njia ziwezekanazo ili wapate madawa ya kimsingi.
Masharti
yanayoamri nchi maskini kufuata Maafikiano juu ya Haki za Kitaaluma
yaliahirishwa kwa miaka kumi. Bali nchi hizi zilikata kujifunga zikikubali
uamuzi unaokwenda kinyume na uwezo wake. Hazikukubali kuwepo kwenyewe kwa hati.
Mjini Geneva, kutafanyika mkutano juu ya uingizaji nchini wa madawa ya ainasafu.
Mapatano haya yangelimalizika kabla ya mwaka wa 2002 kumalizika.
B.
Kuhusu haki ya kila jamii ya kuwa na uhuru juu ya rasilmali yake ya kiasili na
haki ya kupiga vita uharamia pamoja na hati katika uwanja wa viumbe hai, kanuni
ya 19 ya Taarifa yaomba Ushauri wa Maafikiano kuhusu Haki za Kitaaluma,
kuchunguza upya kanuni ya 27 :3 b, kuchunguza utekelezaji wa maafikiano
yahusuyo maafikiano juu ya APIC (…) kuchunguza uhusiano baina ya haki za
kitaaluma na vuimbe hai, ulinzi wa ujuzi asilia, elimu ya kitamaduni na mambo
mengine muhimu… ». Ingawa aya hii yaifungulii milango mapatano mapya juu
ya Haki za Kitaaluma katika Biashara kama ikivyoombwa na Nchi Zinazoendelea,
yaikatai majadiliano juu ya kanuni ya 27 : 3 b), kinyume na
yaliyopendekezwa na Muungano wa Ulaya.
Maendeleo
kuhusu uwanja wa Haki za Kitaaluma katika Biashara (kuhusu madawa) yanayoonekana
katika Taarifa ya Doha yasikiche hali ya kwamba Maafikiano haya hayatajadiliwa
upya. Kutokana na matashi ya viwanda vya kimataifa vya madawa na vya bidhaa za
kilimo, Muungano wa Ulaya na Marekani zakata kata kata kuwepo kwa maafikiano
mapya, kinyume na yanayoombwa na Nchi zinazoendelea.. Hivyo, kazi ngumu zaidi
bado haijafanyika.
C.
Taarifa inatangaza kuanzinshwa kwa majadiliano juu ya kuwepo kwa mfumo wa
kimataifa kujulisha na kuandika hali ya mivinyo na pombe kali. Jambo hili laweka
katika matumizi kanuni namba 23 ya Maafikiano juu ya Haki za Kitaaluma katika
Biashara, haliirekebishi.
DURU
MPYA
Majadiliano
yatafanyika tangu tarehe 01.01.2002 hadi tarehe 01.01.2005. Yataongozwa na
kamati maalum. Mtutano wa mawaziri utachunguza matunda ya majadiliano haya.
Uendeshaji, matunda na utekelezaji wa majadiliano haya utahusu na kufuatwa mara
kwa mara na wanachama wote. Majadiliano haya yatakuwa juu ya nyanja zifuatazo :
-
Haki kwa wote kwenye masoko ya bidhaa zisizo za kilimo : panahusika hapa
ushuru na bei za bidhaa viwandani. Nchi zinazoendelea, hasa hasa zile za
kiafrika, zilikuwa zimependekeza kutokuwepo kwa majadiliano kabla ya uchunguzi
thabiti juu ya athari ya kushusha ushuru na bei kwa kuendeleza viwanda katika
Nchi Zinazoendelea. Sauti ya nchi hizi kaikusikika. Kama hawaangalii makini,
majadiliano juu ya uwanja huu huenda yakasababisha upanishaji mkubwa wa uhuru wa
kibiashara, katika nyanja zihusuzo maendeleo ya kudumu.
-
GATT 1994 (yaani maafikiano yaliyofanywa na GATT ya awali hadi 1994) :
mapatano yatahusu utekelezaji wa kanuni zilizopo, hasa hasa katika uwanja wa
kimisaada (kwa mfano uvuvi) na wa biashara ya kimajimbo.
-
Mazingira : majadiliano yatafafanua uhusiano baina ya kanuni zilizopo ndani
ya Shirika la Biashara Ulimwenguni na maafikiano ya kimataifa juu ya mazingira,
walakini majadiliano haya hayatahusu nchi ambazo hazikutia saini kwenye
maafikiano haya. Hivyo, Marekani bado iko na uhuru wa kutenda itakavyo na
kuamuru wengine kufuata kanuni wasizozitaka. Isitoshe, kufuatana na
inavyoandika, aya yenyewe yafasili, bila kutaja bayana, utiaji fora wa kanuni za
Shirika la Biashara Ulimwenguni katika kanuni nyingine zote za Sheria ya
Kimataifa. Hali kadhalika yashawishi kutounga mkono maafikiano ya kimazingira.
Kufuatana na Taarifa, majadiliano ya kimazingira yatahusu « kupunguza au
kufuta vipingamizi, vihusuvyo bei au la, juu ya bidhaa ama hukuma katika uwanja
wa kimazingira. » Milango imefunguliwa ubinafsishaji kimazingira wa huduma
za kiuma (maji, nguvu, mbolea,…). Kinyume, bali ya kuchunguzwa, mapendekezo
yahusuyo vyeti vya kimazingiza yaliwekwa mikononi mwa kamati maalum. Umuhimu wa
maendeleo ya kudumu haukufafanuliwa kama kipingamizi kwa uenezaji uhuru wa
kibiashara.
-
Utekelezaji. Hapa siyo majadiliano yenyewe juu ya nyanja mpya yanayohusika, bali
mapatano juu ya namna ya utekelezaji wa maafikiano yaliopo. Nyingi mno kati ya
Nchi Zinazoendelea zilikataliwa ombi lake kuchunguza upya maafikiano yaliopo.
Msimamo wa nchi tajiri juu ya Maafikiano katika uwanja wa vitambaa na nguo
haukugusiwa. Wala mbinu za nchi tajiri za kushusha mara kwa mara bei kwa ajili
ya faida zake hazikugusiwa.
-
Marekebisho ya kanuni za usuluhisho wa migogoro. Mapatano haya ndiyo peke yake
yaliyohusu maafikiano yaliopo na jinsi Shirila la Biashara Ulimwenguni
linavyofanya kazi yake. Kinyume na nyanja nyingine za duru mpya, mapatano haya
yatapaswa kumalizika mwezi Mei 2003. Ingawa haiwezekani kujua jinsi mapatano
yatakavyoendeshwa, ni vizuri kuwa kulikuwepo na uwezo wa kuchunguza upya muundo
uliopo, ambao wengi waliupinga.
Katika usiku wa
tarehe 13 na 14 novemba kulijadiliwa aya zifuatazo za Taarifa (20, 23, 26 et
27). Mwanzoni mwa mkutano, Nchi Zinazoendelea ziliwahi kupitisha pendekezo lake
la kuahirisha majadiliano ya nyanja hizi kwenye mkutano wa tano utakaofanyika
katika mwaka wa 2003. Walakini, kutokana na nguvu zilizotumiwa na Muungano wa
Ulaya, nyanja hizi ziliandikwa katika ratiba ya duru mpya, tofauti ikiwa tu
kwamba, kinyume na nyanja nyingine, mapatano juu ya nyanja hizi yataanza
« baada ya mkutano wa tano wa mawaziri, kufuatana na uamuzi
utakaochukuliwa juu ya namna ya kuendesha mapatano. »
Kutokana na kazi
iliyofanywa na India, rais wa mkutano aliandika kwamba : « Ningelipenda
kuandika kwamba baadhi ya wajumbe walipendekeza kufasili zaidi aya za 20, 23, 26
na 27 za mswada taarifa. Kutokana na kuwa katika mapatano haya kunahitajika
kuwepo kwa « makubaliano dhahiri » mnamo mkutano wa 5 wa mawaziri,
msimamo wangu ni kwamba ni bora kuchukua uamuzi dhahiri kabla ya kuanzishwa kwa
mapatano juu ya biashara na utegaji uchumi, biashara na sera za mchuano, uangavu
na soko za raia, kulahisisha biashara. Kutokana na hali hii ya mambo, kila
mwanachama angelikuwa na uwezo wa kuchukuwa msimamo imara. Hivyo, makubaliano
dhahiri yatawahi kuwepo baada ya mkutano wa 5. »
Yaani, katika mwaka
wa 2003, ikiwa Mwanachama fulani hakubaliani na wengine, mapatano juu ya nyanja
hizi nne hayataweza kuanzishwa. Bila shaka, Marekani na Muungano wa Ulaya
zitasisitiza kwamba msimamo huu wa rais hauna maadili ya kisheria, kinyume na
Taarifa yenyewe. Wanasheria huenda wakaamua. Usahihi huu wa rais wa mkutano
uliandikwa katika katika Taarifa ya Doha, na hakuna mashaka juu ya uthabiti wa
taarifa hii. Kadhalika, hakuna yeyote yule ambaye angelijua mkutano
ungelimalizika je, bila usahihi huu uliopendekezwa na rais kabla kupitishwa kwa
taarifa yenyewe. Licha ya mjadala huu juu ya sheria, kunakuwepo msimamo wa
kisiasa wa kutoamuru lolote kwa nchi yoyote ile, kabla ya kuanzisha mapatano juu
ya nyanja hizi.
Nyanja nyingine
ambazo hazitajadiliwa, (biashara ya kielektroniki, uchumi wa viwango vya chini,
madeni na fedha, kubadilishana ufundi sanifu, ushirikiano wa kiufundi na
kuimarisha uwezo) zitachunguzwa na makundi ya kazi ya Shirika la Kazi
Ulimwenguni.
Kifupi,
ingawa muundo na kanuni za Shirika la Biashara Ulimwenguni bado hukandamiza Nchi
Zinazoendelea, nchi hizi zimeanza kutetea haki zake. Mapatano yataendelea, na
yataanzia kwenye nyanja mpya. Kazi
yote itafanyika mjini Geneva. Vita vikali na virefu vitahitakjika ili kuwepo
biashara kwa ajili ya jamii, bali jamii kwa ajili ya biashara.
Mtafiti kwenye Shirika Oxfam Solidarité
(Brussels) na URFIG (Brussels-Paris-Geneva)
21 novemba 2001