Nyaraka zinazotetewa na URFIG kuhusu :

OMC - Shirika la Biashara Ulimwenguni - WTO  

 

 

Taarifa la Geneva (6 juini 2001)

DUNIA YETU SI YA KUUZWA

Shirika la Biashara Ulimwenguni : Lipunguze nguvu ama lifutwe

 

Umewasili muda wa kusimamisha utandalizi na kupigania shughli nyingine ambazo tuna uhakika uhakika zitasaidia kwa kujenga dunia mpya. Kutoka na masauti mengi yasiyo na kifani ya wananchi na serikali tofauti yaliyolipinga, Shirika la Biashara Ulimwenguni lilipoteza nguvu sana. Mkutano wake wa tatu wa mawaziri uliofanyika mjini Seattle (USA) mnamo mwezi novemba 1999, ulimomonyoa uhalali wa shirika hili. Tangu wakati huu, mamilioni ya watu kukoka kwenye nchi maskini au nchi tajiri yamejiunga pamoja na kupiga vita utandalizi kwa ajili ya kujenga hali mpya ya uchumi ambao i haki na ya kutetea.

      Baada ya mkutano wa Seattle, kutokana na kule kupinga uhalali wa shirika la Biashara Ulimwenguni, kulitolea ahadi ya kurekebisha mambo. Walakini, hadi leo, hakuna lolote lile lililofanyika. Bali mambo yaliharibika zaidi. Muda umewasili wa kushusha nguvu na athari za Shirika la Biashara Ulimwenguni. Ukosefu wa demokrasia, ukosefu wa uangavu na wajibu wa shirika hili ambalo lingelipaswa kuendeleza biashara hulu, licha ya wajibu huu, umesaidia kutajirisha wachache, kupaanisha shimo baina ya nchi tajiri na nchi maskini, kufanya maskini jamii za wengi duniani, kuhamisha wakulima na wafanyakazi hasa hasa katika nchi za ulimwengu wa tatu na kuhimiza njia za uzalishaji na za kutumia uchumi zisizodumu.

      Yametupiliwa mbale kinyama malalamiko ya wafanyakazi na wakulima, malalamiko ya wateteyaji haki za binadamu na mazingira, ya viongozi wa kidini na za wazalendo wa nchi tofauti, malalamiko ya Serikali za Ulimwengu wa tatu yanayopinga kutokuwa na ulingano na kuzusha matatizo kunakotokana na na utimilishaji wa duru ya Uruguay.Ofisi ya shughli za utawala wa Shirika la Biashara Ulimwenguni inayojidai kutopendelea upande wowote ule, pamoja na kundi la mataifa tajiri, vile vile na wateteaji wengine wa sera zake, kama kawaida, wanatumia nguvu zao zote zile ili Shirika la Biashara Ulimwenguni linufaishe wana biashara. Mbinu wanayoyitumia ni kusisitiza hali ya kuwa na mtazamo usiojifunga ya Utandalizi. Mapatano yaliyotegemewa kujadili upya maafikiano juu ya ulimaji, huduma, haki za wote kwa kuzalisha mali na biashara yamegeuzwa mwendo. Wana utandalizi hupendelea hasa urekebishaji wa kasoro, jambo ambalo linaharibu zaidi.

      Serikali hudanganywa, ujanja watumiwa ili ukubaliwe mkutano wa nne wa mawazili utakaofanyika nchini Katar tangu tarehe 9 hadi tarehe 13 novemba mwakani. Mapatano mapya ya kupanulia zaidi njia Shirika la Biashara Ulimwenguni yaandaliwa.Maparano haya yamepewa jina la utani la "duru ya maendeleo". Jina hili ni la kuvutia tu. Lengo la kweli la duru hili ni kupanulia wachache, kwa kupitia kwenye shirika la Biashara Ulimwenguni, haki za kuzalisha mali, za kunufaika na masoko ya raia, na sera za mchuano nk.

      Msaada wa namna hii unaopewa mapampuni ya kimataifa utadhoofisha zaidi uchumi wa mataifa na majimbo, wa wafanyakazi, wakulima, wazalendo, manawake na makundi mengine ya jamii. Msaada huu u hatari kwa afya na usalama, mazingira, usalama wa wanyama porini. Matokeo yote haya husababishwa na ukosefu duniani wa msimamo thabiti, mmomonyoko wa uchuni wa kitaifa, shimo kila siku kubwa zaidi kati ya umaskini na utajiri ndani ya kila nchi hata baina ya nchi tofauti. Shanzo cha maafa haya ni utandalizi usio na mipaka.

      Umewasili muda wa kugundua hali ya hatari iwepo sasa biashara ya kimataifa na shirika lake kuu ambalo ni Shirika la Biashara Ulimwenguni. Sasa hivi, mwanzoni mwa karne la 21, hatuna budi kubadili mashirika ya kijadi, ambayo ni si ya haki, bali ni ya kukandamiza. Twapaswa kubuni muundo mpya wa kubadilishana, usiosahau haki za kijamii na ambao ni wa kudumu.

Twaita ulimwengu ili bila kukawia :

- Zilindwe tamaduni za aina mbali mbali, udumu utofauti wa kibiolojia, wa kijamii na wa kiuchumi

- Kuthibitisha hatua kwa hatua sera zinazotilia mkazo biashara na mabadilishano ya kijimbo ; kudhamini haki za kiuchumi, za kijamii na za kitamaduni zinavyojulikana kwa wote.

- Kukarabati uhuru wa jamii tofauti na kudhibiti demokrasia kwa kiwango cha taifa na jimbo.

            Ili mambo haya yatekelezwe, sheria mpya zapaswa kutumika. Sheria hizi zingezingatia udhibitishaji wa demokratia, ulinzi wa mazingira, uadilifu, ushirikiano na tahadhari.

Kutokana na mambo haya, twaomba serikali zetu :

Kutopaanisha Shirika la Biashara Ulimwenguni

            Twaeleza upya upindani wetu kwa kuanzisha upya duru nyingine ya mapatano, upinzani wa kueneza wajibu wa Shirika la Biashara Ulimwenguni kwenye nyanja za uzalishaji mali, sera za mchuano, masoko ya raia, bioteknolojia na uhuru wa viwango vya ushuru wa forodha.

            Kuenea kazi ya Shirika la Biashara Ulimwenguni kwenye nyanja za uzalishaji mali na sera za mchuano, ama kuarmisha mataifa yote kufuata muundo wa Shirika la Biashara Ulimwenguni kuhusu masoko ya raia (mwanzoni uangavu ukiwa ni lazma), kungelikuwa kinyume na uhuru wa kila nchi. Vile vile kungeliweka katika hali ya hatari makampuni madogo na ya kati kati. Kungelishusha maendeleo ya ulimaji na uchumi majimboni. Kungeliathari vibaya jamii na mazingira.

            Hatutaki mbinu mpya zitumiwazo na Muungano wa Ulaya za kuunga mkono mapatano mapya juu ya uzalishaji mali na muchuano katika maafikiano ya kimataifa. Inafaa kwa sasa Shirika la Biashara Ulimwenguni likatazwe kueneza uhuru wa biashara. Badala yake, inafaa lipatikane bila kungoja suluhisho kwa maswala ya dhuluma yanayokumbana nao mataifa ya ulimwengu wa tatu. Hayana uhusiano wowote ule na mapatano juu ya kueneza uhuru wa biashara.

Shirika la Biashara Ulimwenguni li mbali na wajibu wake : Kulinda haki na mahitaji muhimu na kijamii

Kwa nini haki za kijamii na mahitaji muhimu yachunguzwe kwanza na Shirika la Biashara Ulimwenguni ? Jibu hatuna. Maafikiano ya Shirika la Biashara Ulimwenguni hayangelihusu mahitaji ya kijamii au ulinzi wa dunia : chakula, maji, huduma muhimu jamiini, elimu, afya, usalama wa watu, mazingira na ulinzi wa viumbe hai. Kutwaa bila halali kwa sheria za kibiashara katika nyanja hizi kumeishazusha upinzani wa raia dhidi ya viumbe vilivyobadilika kwa vinasaba, dhidi ya uharibifu wa mapori ya asili, dhidi ya upelekaji katika nchi za nje wa vitu vyenye sumu ambavyo vimeishafukuzwa katika nchi vitokamo, dhidi vile vile ya utangazaji wa sifa za tumbaku unaofanywa kinyama na makampuni yake.

VIPI NA MAAFIKIANO MAKUU KUHUSU BIASHARA YA HUDUMA (GATS) ?

WALINDWE RAIA, ZILINDWE HODUMA ZA KIJAMII

Nyanja kama vile afya, elimu, nguvu za umeme na mahitaji muhimu zisilazimishwe kutii kanuni za biashara ya kimataifa. Katika Maafikiano Makuu Kuhusu Biashara ya Huduma (GATS) na katika nyaraka nyingine kumeandikwa kwamba usambazaji wa uhuru wa biashara na uzalishaji mali ngambo vina athari mbaya sana, kwa mfano, kwenye huduma muhimu.

HATUTAKI HATI ZA KUDHAMINI SOKO KWA MAKAMPUNI MACHACHE :

MBEGU NA MADAWA ZI MAHITAJI MUHIMU YA BINADAMU,  SI BIDHAA

Sera zote zihusuzo rasilmali ya kitaaluma zingeliruhusu serikali mbalimbali kutotoa hati zinazoenda kinyume na ulinzi wa afya na usalama. Hati ambazo zingelihusika hasa hasa ni zile zinazohusu madawa na afya. Hati zinazohusu viumbe hai, ikiwa ni vidudu lazma zikatazwe na sheria zote za kitaifa au za kimataifa.

Sheria za leo juu ya rasilimali za kitaaluma zinavyoandikwa katika maafikiano ya kibiashara, kama vile maafikiano juu ya matawi wa rasilimali ya kitaaluma yahusuyo biashara huzuia watu kupata madawa na vitu vingine muhimu. Vile vile huweka mikononi mwa wachache maisha ya viumbe na ujuzi wa zamani, huzuia uhuru wa viumbe anuwai na huwa kipingamizi kwa maendeleo ya kijamii katika nchi maskini kuliko nyingine.

Hakuna haja ya kuingiza haki za rasilimali ya kitaaluma katika maafikiano ya kibiashara.

KUSIWEPO HATI JUU YA VIUMBE HAI    

Sheria za kitaifa na za kimataifa hazina budi kukataza hati zihusuzo viumbe hai na rasilimali ya kitaaluma za aina hii.Utofauti wa vinasaba si mali binafsi ya wamoja. Hivyo, umiliki wa maisha pamoja na wa ujuzi wa kitamaduni ni uharamia. Sharti usimamishwe.

KILA BINADAMU ANA HAKI KWA CHAKULA : USIMAMISHWE UDANGANYIFU JUU YA MAAFIKIANO JUU YA ULIMAJI

Maafikiano juu ya ulimaji hudanganya watu. Msaada kwa ulimaji wa kiwiwanda, ambao umeelekezwa kwenye biashara ya nje, haukupunguzika kamwe. (Bali umeongezwa), ingawa kazi na maisha ya wakulima wadogo wadoko hudhoofishwa na uhuru wa kuingiza bidhaa.

Ili wakulima hawa wasisahaulike, hatuna budi kupunguza sana msaada kwa biashara ya nje ya mazao ya kilimo, na kutazama upya uhuru katika uingizaji wa bidhaa.

Hatua za kulinda walimaji wadogo wadogo zisirudishwe nyuma na sheria za biashara ya kimataifa.Muundo wa kibiashara usiharibishe kiwango cha maisha ya wakulimu wadogo, wavuvi na raia wananchi.

Haki za kila mtu kwa chakula haziwezi kuwepo ikiwa uhuru kwa chakuli haudhaminiwi, yaani haki ya kila jamii kwa kujichagulia sera pekee kuhusu chakula na kilimo, pamoja na haki kujitaftia chakula kufuatana na mila na tamaduni zake.

KUSIWEPO HURIA KATIKA KUTEGA UCHUMI.

Maafikiyano ya Shirika la Biashara Ulimwenguni juu ya vitegauchumi vinavyohusu biashara hayana budi kubadilishwa. Mataifa yote, hasa hasa yale maskini, hupaswa kujichagulia sera ambazo zinahimiza uzalishaji mali wa kizalendo na kuendeleza viwanda vidogo vidogo vya kitaifa kwa ajili ya maendeleo. Kubadilishwa kwa maafikiano haya kusiunge mkono wajibu wa Shirika la Biashara Ulimwenguni katika uwanja wa kutega uchumi. Ndiyo maana twapinga na kukata katakata maafikiano mapya ndani ya Shirika la Biashara Ulimwenguni juu ya sheria za vitegauchumi, juu ya muundo wa kutega uchumi au juu ya utegeji uchumi wowote ule.

Mapendekezo kama yale ya Maafikiano Makuu Kuhusu Biashara ya Huduma (GATS) ama yale yanayodai kutumia uangavu katika uwanja wa kutega uchumi, au yale juu ya maafikiano yanayojumuisha nchi nyingi ni mbinu tu za kiujanja zenye lengo la kushawishi mataifa au mashirika yaliyokata kuunga mkono maafikiano ya kiujumla juu ya vitegauchumi. Shabaha lenyewe ni kunufaaisha wategani uchumi kutoka ugenini. Twatupilia mbali mbinu zote hizi ambazo hasha hazitofautiani na MAI.

KWA AJILI YA USAWA KATIKA UFANYAJI BIASHARA  :

TOFAUTI NA UPEKEE KATIKA VITENDO

Kaika biashara ya kimataifa, inafaa uzingatiwe umaskini wa mataifa ya ulimwengu wa tatu. Bila haki hii, nchi maskini kamwe hazitafaidika kwa biashara ya kimataifa.

KWANZA HAKI ZA KIJAMII NA MAZINGIRA

Huria ya biashara hupendelea faida ya makampuni kuliko ile ya raia na mazingira. Tuna haja ya biashara inayofanyika kwa kutovunja haki za watu. Vile vile, inafaa ziheshimike haki za binadamu pamoja na haki za wafanyakazi, bila kusahau zile zinazohusu mazingira, afya, elimu, haki za wazalendo, haki za kimaendeleo, zile zinazohusu usalama wa watu, usalama wa chakula na usalama wa wanyama wa porini.

Kwa mfano, azimio la Shirika la Kazi Duniani (ILO) juu ya haki za kimsingi kazini, Maakala juu ya viumbe anuwai, itifaki juu ya usalama wa kibiolojia pamoja na azimio la Umoja wa Mataifa juu ya haki za binadamu hupaswa kufanikishwa ifaavyo.

Ili zifanikishwe haki wafanyakazi na haki nyingine za binadamu, hatunabudi kushawishi mashirika ya kimataifa yanayohusika.

TWAAKA KUWE NA DEMOKRASIA KATIKA KUFANYA UAMUZI  

Jamii zina haki ya kujichagulia mfuno wa kimaendeleo na zina haki ya kujulishwa yanayofanyika katika uwanja wa biashara ya kimataifa. Jamii hizi zaomba kujulishwa jinsi uamuzi unavyofanya katika maafikiano. Jamii hizi zataka pia kuwe uangavu, demakrasia na mfungamano katika shughli za mashirika ya kimataifa. Shughli za Shirika la Biashara Ulimwenguni zaendeshwa kisiri na hazishirikishi nchi nyingi na kusahau wataalamu wasiotegemea serikali. Shirika la Biashara Ulimwenguni limewekwa mikononi mwa serikali chache, ambazo vile vile kwa upande wake zi mikononi mwa makampuni beberu ya kimataifa.

KUPINGA MUUNDO MWENYEWE     

Tawi la Shirika la Biashara Ulimwenguni la kutatua migogoro la kukubaliwa : latumia muundo ambao si halali wa sheria zisizona haki. Kadhalika, muundo huu wakosa demokrasia. Pia hujichukulia kwa nguvu wajibu wa kutunga na kutiisha sheria, wajibu ambao kwa kawaida u wa nchi huru au majimbo totauti.

Ili muundo wa biashara ya kimataifa uwe halali, inafaa pia kuwe na mabadiliko ya maana nje ya Shirika la Biashara Ulimwenguni. Muundo kama huu hauna budi kuzingatia kwanza haki na ubora wa maisha vya wafanyakazi na wakulima ambao huzalisha bidhaa na huduma. Hakuna serikali ama shirika la kimataifa ambalo lingeliruhusiwa kujisahaulisha jinsi mashirika ya kimataifa na serikali furani zinavyoshambulia haki za kimsingi za wafanyakazi na zinavyodharau haki zilizoishatambuliwa na wafanyapazi, bila kusahau upotovu wa usalama wa kazi na jinsi mishahara inavyopunguzwa. Lazima, popote pale ulimwenguni, haki za wafanyakazi zikazwe.

Vile vile, sharti Shirika la Kimataifa la Fedha, Benki ya Dunia na benki nyingine za kimaendeleo zifute 100% madeni ya nchi maskini, ili nchi hizi zipambane na umaskini mwenyewe. Ratiba za kurekebisha kimuundo hali ya uchumi zenye lengo la kuleta huria zinapaswa kusimamishwa. Inafaa, katika Umoja wa Mataifa, serikali zijadili kidemokrasia ili kuwe maafikiano yanayolazimisha makampuni ya kimataifa hutovunja haki za binadamu, mazingira na demokrasia.

HITIMISHO NA MATOKEO   

Sisi, tunao piga sahihi kwenye taarifa hili, tumejituma kutumia nguvu zetu zote ili biashara ya kimataifa ifanyike ifaavyo, iwe halali kijamii na ichungwe kidemokrasia. Twaia serikali zetu ili zitafute masuluhisho bora kwa maswala tuliyoyataja hapa juu na kupungua ubeberu wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Lazima Serikali hizi zirekebishe kinaganaga uundo wa Shirika hili. Twajituma kuija raia wa nchi zetu ili wajiunge nasi ili maswali yetu yajibike na ipangue sera bovu ya Shirika la Biashara Ulimwenguni.Tutaunga mkono watu wengine ambao kama sisi, huendesha kampeni za kutetea umoja wa kimataifa. Twajituma kueneza popote pale duniani ari ya Seattle na kuzuia Shirika la Biashara Ulimwenguni kuanzisha wa duru mpya ya mapatano ambao inatarajika huko Katar.

 

(Maarifa yaliyopigiwa sahihi na mamia ya mashirika kutoka pembe zote za dunia, kukiwemo URFIG)

 

Déclaration de Genève - Notre monde n'est pas à vendre - OMC : la soumettre ou la supprimer (6 juin 2001)