Nyaraka zinazotetewa na URFIG kuhusu :

OMC - Shirika la Biashara Ulimwenguni - WTO

 

 

 MSWADAJARIJIO WA KASHFA WA TAARIFA MAALUM YA MKUTANO WA MAWAZIRI WA SHIRIKA LA BIASHARA ULIMWENGUNI

(Oktoba 30, 2001)

 

Mswadajaribio ambao hivi karibuni uliandikwa kwa ajili ya mawaziri wa Shirika la Biashara Ulimwenguni waja kama maafa kwa nchi maskini na kwa nchi zinazoendelea. Vile vile mswadajaribio huu wapuuza mapendekezo ya shirika la raia wa ulimwengu

Shirika la Biashara Ulimwenguni halina demokrasia yoyote ile. Mswada wapitishwa kwa nguvu ili ujadiliwe katika mapatano yanayotarajika, ingawa wapingwa na wanachama wengi wa Shirika la Biashara Ulimwenguni pamoja na waakilishi wa raia.

Leo, makundi ya waakilishi wa raia kutoka kwenye pembe zote za dunia wametupilia mbali mswadajaribio wa taarifa ya mawaziri watakaokutania jijini Doha kwenye mkutano wa Shirika la Biashara Ulumwenguni. Msadajaribio wa nyaraka ya kutumiwa kwenye mkutano wa Shirika la Biashara Ulimwenguni unaotarajika tangu tarehe 9 hadi tarehe 13 Doha, nchini Katar, haukukubaliwa na wawakilishi wa raia.

Hali kadhalika, nchi maskini ambazo zahisi dharau hazina imani kwenye mswada huu huu ambao waandikwa kama vile wanachama wote wameisha kubaliana juu ya ajenda mpya ya Shirika la Biashara Ulimwenguni, jambo ambalo si la kweli.

MaNGO’s kutoka kwenye pembe zote za dunia yaomba mataifa tofauti yatokamo kupinga nyaraka hii ambayo si halali. Mashirika haya yataka mataifa yazuie mswada huu kutumiwa katika mkutano wa Doha wa mawaziri wa Shirika la Biashara Ulimwenguni.

Nyaraka hii imeandikwa baada ya mswaada mwingine ambao ulitupiliwa mbali na wajumbe wa nchi maskini ambazo ni wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Nyaraka mpya, kama ile ya kwanza, haizingatii mapendekezo muhimu ya nchi zinazoendelea, bali huingiza mambo mengi yaliyopingwa na nchi hizi ambazo ni wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni.

Mashauriano ambayo mwezi jana yalifanyika kwenye Shirika la Biashara Ulimwenguni yalisababisha nyufa zaidi, yalipopendekeza mswada ambao kaurekebishi kamwe nyaraka inayopingwa na wengi.

Hali hii ya mambo yapaanisha ufa katika ukosefu wa demokrasia ndani ya mfumo wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Miezi mingi imepita wengi kati ya wanachama binafsi wa Shirika la Biashara Ulimwenguni wakikataliwa kupitisha mapendekezo yao.

Kinyume na yanaoandikwa katika nyaraka, nchi wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni hazikubaliani juu ya ajenda ijao ya shirika hili. Hata tangu kabla ya mkutano wa Seattle wa mawaziri wa Shirika la Biashara Ulimwenguni, nyingi kati ya nchi zinazoendelea zimeomba kushughlikiwa kwa dosari na ukosefu wa haki ndani ya Shirika la Biashara Ulimwenguni.. Walakini Marekani imekuwa kipingamizi.

Muungano wa Ulaya, kwa upande wake, unatetea kuziidishwa kwa nyanja zinazoshughlikiwa na Shirika la Biashara Ulimwenguni, kama vile utegaji uchumi, sera ya mchuano, jambo ambalo halikukubaliwa na nchi zinazoendelea

Upinzani mkubwa waonekana pia juu ya mambo kuhusu ulimaji. Kwa niaba ya nchi zinazoendelea, lazma mkazo utiliwe kwenye kutosha kwa chakula na maendeleo ya vijiji. Marekani na Muungano wa Ulaya hupendekeza zaidi kulindwa kwa masoko yake, kukiwapo misaada na mikopo ya mahuruji.

Ingawa mengi kati ya mataifa wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni yataka majadiliano mapya juu ya sera za kukataza ujazaji wa bidhaa rahisi katika soko, Marekani haitaki kusikia pendezo hili. Hali tofauti, katika mswada mpya, nyanja kama vile utegaji uchumi, na sera za mchuano zilipewa nafasi kubwa kwa ajili ya mapatano yajayo.

Kinyume, katika mswada mpya, orodha ya mapendekezo ya nchi wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni ambazo si tajiri imefutwa. Katika mapendekezo haya, nchi zinazoendelea zatangaza mambo ya kuchunguza upya ama ya kurekebisha kabla ya majadiliano mapya ndani ya Shirika la Biashara Ulimwenguni.

Kutokana na maafikiano yanayotumiwa sasa katika Shirika la Biashara Ulimwenguni, hisa ya nchi maskini kuliko nyingine katika biashara ya kimataifa ilipunguka. Hali kadhalika, sera za nchi hizi kuhusu nyanja kama maendeleo na afya zimeshambuliwa, eti zavunja sheria ya Shirika la Biashara Ulimwenguni.

Mswadajaribio mpya wanuufaisha Marekani, ukisisitiza kwamba hakuna limoja kati ya mambo haya litakalochunguliwa, ikiwa nchi zinazoendelea hazilegezi mapendekezo yake.

Mswadajaribio mpya wadharau pia wawakilishi wa raia ya wakulima, wavuvi, wafanyakazi na wenye kutetea hali safi ya mazingira, ambao, kutoka nchi tofauti, walijadiliana na kufanya kazi ya pamoja tangu miaka mingi kabla ya mkutano wa kiwaziri wa Seattle, hadi leo.

Makundi mengi ya wawakilishi wa raia na ya wafanyakazi wamejiunga pamoja na kusema : “Dunia Yetu Si ya Kuuzwa : kampeni ya kutekea kurekebishwa ama kufutwa kwa Shirika la Biashara Ulimwenguni”. Kampeni hii yaita wanachama ili wafikiri juu ya kuwepo kwa Shirika la Biashara Ulimwenguni halili.

Mapendelezo ya makundi haya ambayo yanaundwa na mashirika kukoka kwenye nchi zinazoendelea na nchi tajiri, mashirika ya wafanyakazi na ya wakulima vile vile yalipuuzwa katika mswadaratibio mpya ulioandaliwa kwa ajili ya mkutano wa mawaziri.

Ukaidi wa Ofisi ya Shirika la Biashara Ulimwenguni na wa nchi chache tajiri ambazo hushawishi Shirika la Biashara Ulimwenguni kutozingatia mapendekezo ya nchi zinazoendelea na ya wawakilishi wa raia utaufanya mkutano wa kiwaziri wa Doha uletee balaa mengi kati ya mataifa yatakayo hudhuia mkutano huu, au utaufanya mkutano huu ushindwe kama vile ulivyoshindwa mkutano wa Seattle: ukataji hapo hapo au taarifa batili

Wenye kutia sahihi kwenye taarifa

 

*Alliance for Democracy, U.S.

Wasiliana na Ruth Caplan (Washington DC): 202-244-0561

*Arab NGO Network for Development, Lebanon

Wasiliana na Ziad Abdel Samad (Beirut): +961-1-319-366

*ECOROPA, France

Wasiliana na Agnes Bertrand (Sauve): 33-4-66-77-0704

*Focus on the Global South, Thailand

Wasiliana na Aileen Kwa (Geneva): 41-22-791-8050

*Friends of the Earth – International

Wasiliana na Alexandra Wandel (Brussels) +32-2-542-0185 au Ronnie Hall (London) +44-1243-602-756


*Global Exchange, U.S.

Wasiliana na Juliette Beck (San Francisco): 415-255-7296 x 254

*IBON Foundation, Philippines

Wasiliana na Tony Tujan (Manila): +632-714-1580

*Institute for Agriculture and Trade Policy, U.S.

Wasiliana na Shefali Sharma (Geneva) +41-22-789-0724 na Sophia Murphy

(Minneapolis) +612-870-3454

*Institute for the Re-localization of the Economy, France

Wasiliana na Agnes Bertrand (Sauve): 33-4-66-77-0704

*Public Citizen, U.S.

Wasiliana na Margrete Strand (Washington DC): +202-454-5106

*Via Campesina, International

Wasiliana na Nico Verhagen (Brussels): +32-2-343-8444

*URFIG (Unité de Recherche, de Formation et d'Information sur la Globalisation - Ofisi ya Utafiti, Ushauri na mMarifa juu ya Utandalizi)

Wasiliana Raoul Marc Jennar (Brussels) : 32  478 913 812

 

THE DESASTROUS LATEST DRAFT OF WTO MINISTERIAL DECLARATION