Nyaraka
zinazotetewa na URFIG
OMC -
Shirika la Biashara
Ulimwenguni - WTO
Nchi
Maskini zatangaza kutokuwa tayari
kwa
duru mpya ya mapatano ya kibiashara
na
Mwenyekiti
Habari
juu ya Biashara katika Afrika ya Kusini na ya Mashariki na Uamuzi
wa Mapatano
(Southern
and Eastern African Trade Information and Negotiations Initiative-SEATINI)
(Makala
iliyotangazwa kwenye
http://wtoaction.org/discuss)
Tangu
tarehe 22 hadi tarehe 24 Julai 2001, mataifa 49 ambayo ni maskini kuziidi
mengine yamekutania Zanzibar na kwa sauti moja yakatangaza kwamba hayatashiriki
kwenye duru mpya ya mapatano ya kibiashara ambayo yatarajika kufanyika huko
Doha.
Baada
ya kushindwa kwa mkutano wa Shirika la Biashara Ulimwenguni uliofanyika mjini
Seattle, mataifa tajiri, hasa hasa yale ya Muungano wa Ulaya, yajaribu
kushawishi nchi maskini kuunga mkono duru mpya.
Huko
Zanzibar, nchi maskini hizi, zote kwa pamoja, zilitangaza kuwa « …Kutokana
na uhaba wa nguvu za nchi maskini, mapatano ya kibiashara ya kimataifa
yatazingatia ukosefu huu wa nguvu ambao unasababisha kutoweza kwa nchi hizi
kushiriki ifaavyo kwenye mapatano haya yenye ajenda pana. Vile vile nchi hizi
hazitaweza kufuata masharti mapya» (Ratiba ya maendeleo ya nchi maskini kwa
ajili ya mkutano wa 4 wa Mawaziri wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Mkutano
huu ni wa kujadili juu ya malengo na mapendekezo – LDC/MM/ZNZ/3, 24 julai
2001).
Katika
hotuba yake ya kufunga mkutano, Bwana Iddi Simba, Waziri wa Viwanda na Biashara
wa Tanzania alifafanua hali ya mambo : « Kufuatana
na jinsi tulivyoelewa, lengo la nchi tajiri ni kuanzisha huko Doha
duru mpya ya mapatano ya kimataifa na ya kibiashara. Nyingi miongoni mwa
nchi maskini zingependa zaidi kurekebisha na kutekeleza maafikiano ya duru ya
Uruguay na kuendeleza mapatano juu ya utathmini wa maafikiano haya na ajenda ya
muundo wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Wengi kati yetu hatuwi tayari kwa
duru mpya. Kwa niaba yetu, kuna sababu nyingi za kupinga duru mpya. »
Kwa
mfano, nchi maskini zaogopa vikwazo ambavyo huenda vitafuata kutoweza kuheshimu
masharti mapya ambamo nchi hizi zitakuwa zimejiingiza «Shirika
la Biashra Ulimwenguni ni ofisi ya mapatano ambayo huzaa masharti na kubuni
vikwazo kwa wale wasioyaheshimu masharti haya. Hatuna budi kuwa na makini kabla
ya kutoa uamuzi juu ya masharti mapya. Hali kadhalika, twapaswa kukataa
kuingizwa kwa nguvu ndani ya duru mpya ambayo wengi kati yetu hawawezi hata
kufafanua. U mpana wajibu unaotokana na Muundo Wa Biashara ya Kimataifa ( Système
Commercial Multilatéral -SCM). »
Katika
maandiko ya mwisho ambamo kuna « Malengo na Mapendekezo ya Mapatano»,
wajumbe wa nchi maskini wamebadilishana mawazo juu ya maswala matato muhimu :
soko kwa wote, utekelezaji wa maafikiano na ajenda. Huhusu soko, mkazo ulitiliwa
kwenye Mashati ya Asili. Bangladesh, ikisaidiwa na Nepal pamoja na Bhutan,
zimetaka Masharti haya yawe na « huria » ili kila nchi ijichagulie
soko kwa njia halali.
Bali,
wajumbe wengi walipinga neno « huria ». Baada ya mazungumzo ya muda
mrefu, wajumbe wamekubaliana kubadili neno « huria » na kutumia
« halisi na legevu. ». Vivyo wajumbe walikubaliana na umoja ukarudi
ndani ya kundi la nchi maskini.
Walikubaliana
pia kutumia popote maneno bora zaidi na kubadili neno « huria ».
Rais amefasili kwamba, kwa niaba ya nyingi kati ya nchi maskini, hiria
ilirudisha nyuma maendeleo ya viwanda na kuziidisha umaskini na ukosefu wa kazi.
Neno «Hulia » limegeuka kama matusi katika msamiati wa nchi maskini au wa
nchi zinazoendelea kwa ujumla.
Kuhusu
utekelezaji wa maafikiano yaliopo, wajumbe wameandika maswala ambayo « wanatumaini
kutatua kabla, mnamo na baada ya mkutano wa Doha ». Miongoni mwa maswala
haya kuna mambo yanayopaswa kufanywa na nchi maskini katika uwanja wa kilimo,
huduma misaada SPS na TBT, vitambaa vya nguo, maafikiano MIC, ADPIC, utathmini
wa utathmini wa forodha, shughli za kupinga uzajazi wa bidhaa rahisi katika soko
na fidia pamoja na hifadhi : « Nchi maskini
ziepushwe na hifadhi yoyote ile. Nchi maskini ambazo zatumia hifadhi lazma
zisifuate fidia. »
Kuhusu
ajenda ambayo inatarajika kujadiliwa Doha, nchi maskini zimeonyesha msimamo wake
juu ya ulimaji, biashara ya huduma pamoja na haki za asilimali ya kitaaluma.
Baadhi ya kanuni zinazoandikwa katita haki hizi za kiataaluma zitarekebishwa
upya katika mkutano wa Doha. Msimamo wa Nchi Maskini juu ya kanuni ya 27.3b ni
huu ufuatao : urekebishaji wa kanuni hiyi utapaswa kutilia mkazo kwa
« kutotoa hati yoyote ile » iliwa inahusika mimea, wanyama, sehemu
za mimea na za wanyama, ikiwemo utafiti wa kivinasaba na kibiologia kwa ajili ya
kupata mimea, wanyama, na sehemu zake. Sasa i wazi kuwa hati kuhusu viumbe hai
zimetupiliwa mbali. Wajumbe
walitangaza pia kwamba : « utoaji wa hati juu ya madawa wa kimsingi
kufuatana na orodha ya Shirika la
Umoja wa Mataifa linaloshughlika na Afya zapaswa kukatazwa».
Miongoni
mwa wajumbe waliokutania Zanzibar kulikuwa Nchi Maskini nyingi ambazo ambazo si
wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni. Nyingi kati ya nchi hizi ziliomba
kuwa wanachama na bado hazijaingizwa ndani mwa Shirika hili. Tangu 1997, nchi
maskini sana zimekubaliwa kuwa wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni.
Sababu ni kuwa ugumu ughali na masharti mengine ya kukubaliwa kuwa mwanachama wa
Shirika la Biashara Ulimwenguni. Huko Zanzibar,
Nchi Maskini zilipendekeza kuwa : « Kutokana na hali ya kipekee ya uchumi,
ukosefu wa fedha, umaskini wa kibiashara na kutoendelea kwa Nchi Maskini, katika
mapatano wa kuingizwa, wanachama wa Shirika la Biashara Ulimwenguni wangelipaswa
kutoshurtisha mengi juu ya asilimali ama huduma zinazokuwa katika Nchi Maskini,
kufuatana na na mapendekezo ya Mkutano wa Mawaziri yanayozitetea nchi hizi. »
Nchi
Maskini zapendekeza kwamba katika mapatano ya Doha mambo mawili yatiliwe mkazo
zaidi. Jambo la kwanza ni kuwa hali ya kila nchi maskini ichunguzwe kipekee.
Jambo la pili linahusu msaada wa kitaalamu ambao utazisaidia nchi maskini
kujadiliana na nchi nyingine ifaavyo katika mapatano ya kisasa na kuweza
kushiriki katika muundo wa biashara ya kimataifa.
Kinyume
na yanayopendekezwa na nchi tajiri ili yajadiliwe huko Doha, Nchi Maskini hazi
zilizokutania Zazimbar hazikutaja sana « nyanja mpya ». Miongoni mwa
nyanja hizi mpya ambazo nchi tajiri zingelipenda sana zipewe nafasi kubwa kwenye
ajenda ya Doha kuna zile zilizochaguwa katika mkutano wa Singapore, yaani
biashara na utegajiuchumi, sera za mchuano, uangavu katika soko za kiraia,
urahisi katika mabadilishano. Vile vile kuna zile zilizochaguliwa katika mkutano
wa Geneva na nyanja nyingine kama vile kanuni za kazi, mazingira na bei
iviwandani.
Nchi
Maskini zilifafanua kutohusika kwake na nyanja hizi. Hali kadhalika, nchi hizi
zilitangaza ukosefu wake wa uwezo «kivifaa, tiufundi na kisaikolojia »,
ili ziendeshe mapatano juu ya nyanja hizi (kama alivyosema rais).
Kwa niaba ya nchi maskini, maswala juu ya vitegaji uchumi, sera za
mchuano na uangavu katira soko za kiraia zachunguzwa sasa katika makundi tofauti
ya kikazi za Shirika la Biashara Ulimwenguni. Kazi za makunzi haya bado
hazijamalizika, ndiyo maana hakuna haja sasa ya kuanzisha mapatano mapya juu ya
nyanja hizi
Msimamo
wa Nchi Maskini kuhusu « biashara na mazingira » ulikuwa wa kuunga
mkono mapatano yanatoendeshwa sasa na Kamati ya Biashara na Maendeleo. Nchi hizi
zatangaza kwamba mapatano haya ya muhima. Sharti yaendelezwe. Bali nchi maskini
zilionya kwamba ulinzi wa kimazingira usitumiwe dhidi ya bidhaa kutoka kwenya
nchi maskini».
Biashara
pekee yake si lengo. Ni kifaa ni kifaa cha kutoa kwenue umaskini na kuwekwa
kando wale amabao ni maskini na wamewekwa kando katika jamii ya dunia. Nchi
maskini na nchi tajiri zote zakubaliana kwa jambo hili. Katika bara la Afrika,
nchi ambayo yasemekana imeendelea ni Afrika ya Kusini (wanaotaja nchi hii
wajidanganya). Kabla ya mkutano wa Zanzibar, Afrika ya Kusini iliita nchi zote
wanachama wa SADC katika mkutano wa Johannesburg. Lengo la mkutano huu lilikuwa
ni kuhimiza nchi za SADC kukubali duru mpya la Doha. Kama nchi tajiri, Afrika ya
Kusini inadai kwamba duru mpya itazisaidia nchi maskini. Bali, katika mkutano wa
Zanzibar, Nchi Maskini, angalau zile ambazo zi wanachama wa SADC (ikiwamo
Tanzania, Uganda, Zambia na Lesotho), zote kwa pamoja, zilikata katakata duru
mpya la Doha.
Mara
nyingi jamii tajiri zilijituma kukusaidia jamii maskini zaidi ulimwenguni. Huko
Zanzibar zilisikika sauti za wale ambao ni maskini. Wajumbe walishangilia
mkutano wa Nchi maskini huko Zanzibar. Mkutano huu ulithibitisha umoja wa
mataifa 49 maskini zaidi ulimwenguni. Umoja huu unatafsiri vile vile maoni ya
mataifa haya juu ya mkutano wa Doha.
Swali
linalobadi ni kujuwa kama huko Doha, nchi tajiri zitalisikia sauti hili la nchi
maskini.
Zanzibar 24 julai 2001
Les
Pays les Moins Avancés (PMA) déclarent